Breaking News

LADY JAY DEE AZINDUA MAJI YENYE JINA LAKE

MWANAMUZIKI wa kizazi kipya Bongo, Judith Wambura (Lady Jay Dee) pichani, mapema leo amezindua maji yenye jina lake katika hafla ilifanyika Paradise City Hotel, jijini Dar es Salaam. Akiongea katika uzinduzi huo, Jay Dee alisema kwamba, anatarajia kuyaingiza maji hayo mtaani kuanzia Januari Mosi, 2011, na yatauzwa kwa bei ya kawaida. Alielezea pia namna atakavyoendesha shughuli zake za kibiashara na sanaa kwa ujumla. Akifafanua zaidi, alisema bendi yake itapunguza shoo ambapo sasa atapiga siku moja tu kwa wiki tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Maonyesho hayo yatakuwa yakifanyika kila siku ya Ijumaa katika ukumbi wa Mzalendo Pub Millennium Tower Kijitonyama, jijini Dar es Salaam. Pia Jay Dee, ambaye anakuwa mwanamuziki wa kwanza nchini kuwa na jina kwenye bidhaa kama maji, aligusia sula la kufanya kazi za kimataifa zaidi, likiwemo la kuingia mkataba na kampuni ya Rock Star, ambayo itasimamia kazi zake za muziki kwa muda wa miaka mitano.

Alimalizia kwa kusema kuwa mwanzoni mwa mwaka ujao, anatarajia kufungua mgahawa wake mkubwa maeneo ya Kinondoni-Morocco jijini Dar es Salaam, ikiwa ni moja ya mipango yake ya kimaendeleo kwa mwaka 2011.
Maji yaliyozinduliwa yakionyesha lebo yenye jina la Lady Jay Dee, muda mfupi kabla ya mchakato huo kuanza.
..maji na matamu!
Meneja wa Lady Jay Dee ambaye pia ni mumewe, Gardner Habash, akifafanua jambo katika uzinduzi huo.
Mwakilishi wa MTV na Rock Star Tanzania, Christine Mosha ‘Seven’ akifafanua jinsi mkataba wa JayDee na kampuni hiyo ulivyo.
Baadhi ya waandishi wa habari wa kike kutoka vyombo mbalimbali wakiwa kwenye pozi la pamoja.
Mpiga picha wa kampuni ya Habari Corporation, Muhidin Sufiani, akitimiza wajibu wake katika uzinduzi huo.
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Jaffary Mshamu ‘Jaffaray’ (katikati), akiwa kwenye pozi na baadhi ya wadau waliofika kushuhudia uzinduzi huo.
Mwanamitindo Fideline Iranga (kushoto), akiwa kwenye pozi na mwanamitindo wa kimataifa, Flaviana Matata, muda mfupi baada y
Lady Jay Dee wa (tatu kulia), akiwa kwenye pozi na baadhi ya waalikwa baada ya uzinduzi huo.
Afisa Uhusiano wa benki ya NMB, Shyrose Banji (kushoto), akiwa kwenye pozi na mtangazaji wa Star TV, Sauda Mwilima.
Baadhi ya wanahabari wakipata chakula cha mchana baada ya uzinduzi huo.

How about this Article

No comments:

Leave a Reply