Breaking News

UJASILIAMALI NA MAANA YAKE



Kwa sasa ni jina maarufu sana hapa Tanzania, mtu yeyote aliyefanikiwa katika biashara hupewa jina hili. Maana ya ujasirimali inabaki katika uwezo wa kufanya maamuzi sahihi wa kutumia rasilimali chache zinazokuzunguka vizuri ili uweze kupata faida.

Mathalani rasilimali zinazokuzunguka ni ardhi, watu na maji, ni vipi mchanganyiko huu utautumia vizuri ili uweze kupata zao (output) ambayo itakusaidia kujikwamua katika hali uliyonayo. Ama ni vipi utatumia mtaji mdogo ulionao kufanya biashara itakayokuletea faida ambayo utaitumia kuongeza mtaji na kuikuza biashara yako.

Fahamu kwamba lengo lolote la mjasiriamali ni kupata faida na kumridhisha mteja ambaye anatumia bidhaa ama huduma inayotolewa na mjasiriamali. Bidhaa ama huduma ndio msingi wa mjasirimali yeyote ambaye anataka kupata faida. Mathalani mkulima wa mahindi bidhaa yake ni mahindi hivyo atauza mahindi kujipatia faida, na mtabibu wa mifugo anatoa huduma ya matibabu kwa mifugo na kulipwa ujira kwa kutoa huduma hiyo.

How about this Article

No comments:

Leave a Reply